Embakasi ni mtaa wa Nairobi, mji mkuu wa Kenya. Uko mashariki mwa katikati ya jiji. Ni mtaa wa makazi na wengi wa raia wanaoishi humo ni wa mapato ya daraja la pili la wastani. Ni kata ya eneo bunge la Embakasi Mashariki, kaunti ya Nairobi.
Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, uwanja wa ndege mkuu Nairobi uko Embakasi na ulijulikana kama Embakasi Airport wakati ulipofunguliwa mwaka wa 1958.