Kialawa ni lugha ya Kigunwinyguan nchini Australia inayozungumzwa na Waalawa katika jimbo la Northern Territory. Isichanganywe na lugha ya Kialagwa nchini Tanzania.
Katika sensa ya mwaka 2006, idadi ya wasemaji wa Kialawa ilihesabiwa kuwa watu kuminawawili tu, yaani lugha imekaribia kutoweka hivi karibuni. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kialawa kiko katika kundi la Kimaran, yaani inahusiana na lugha ya Kimara.