Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Nyuki-kekeo

Nyuki-kekeo
Coelioxys froggatti
Coelioxys froggatti
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Hymenoptera (Wadudu wenye mabawa mangavu)
Nusuoda: Apocrita (Hymenoptera wenye kiuno kipana)
Familia ya juu: Apoidea
Latreille, 1802
Ngazi za chini

Familia 3 zenye nyuki-kekeo na jenasi 8 katika Afrika ya Mashariki:

Nyuki-kekeo (kutoka kwa Kiing. cuckoo bees) ni nyuki waliotaga mayai yao katika viota vya nyuki wengine, kama vile kekeo hufanyia ndege wengine. Kuna makundi mbalimbali ya nyuki-kekeo. Jenasi iliyoenea zaidi na kuwa na spishi nyingi barani Afrika ni Coelioxys ya familia Megachilidae yenye spishi 21 katika Afrika ya Mashariki. Jenasi nyingine ya familia hii, Euaspis, ina spishi chache, ambazo moja tu imerekodiwa kutoka Afrika ya Mashariki. Makundi mengine hutokea katika familia Apidae, muhimu zaidi duniani kote ikiwa nusufamilia Nomadinae yenye spishi 14 katika Afrika ya Mashariki. Kabila Melectini ina spishi 20 za Afrika ya Mashariki katika jenasi Afromelecta na Thyreus. Makabila mengine nne zilizo na nyuki-kekeo hazipatikani Afrika (Bombini, Ericrocidini, Euglossini na Isepeolini). Katika familia Halictidae jenasi Sphecodes ina spishi 6 za nyuki-kekeo katika Afrika ya Mashariki.


Previous Page Next Page






Пчолы-зязюлі BE Пчолы-зязюлі BE-X-OLD Kukaččí včely Czech Cuckoo bee English Abeja cuco Spanish Abeille coucou French Կկու մեղուներ HY Пчёлы-кукушки Russian Cuckoo bee SIMPLE

Responsive image

Responsive image