Utiifu, katika maisha ya binadamu, ni aina ya "mwenendo ambayo mtu anafuata maelekezo au maagizo ya wazi aliyopewa na mwenye mamlaka".[1]
Ni tofauti na mtu kufuata athari ya wenzake au mkondo wa umati.
Kimaadili utiifu unaweza kutazamwa kwa namna mbalimbali, chanya au hasi, hasa kulingana na uadilifu au uovu wa agizo lenyewe, kwa mfano lile la Hitler kuhusu mauaji ya kimbari ya Wayahudi.[2]