Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Bahari ya Java

Ramani ya Bahari ya Java.
Pwani ya Bahari ya Java karibu na Anyer

Bahari ya Java ni sehemu ya bahari iliyopo kati ya visiwa vya Indonesia vya Borneo upande wa kaskazini, Java upande wa kusini, Sumatra upande wa magharibi, na Sulawesi upande wa mashariki.

Mlangobahari wa Karimata upo kwenye kaskazini magharibi na kuiunganisha na Bahari ya Kusini ya China.

Eneo lake ni la km² 320,000.

Uvuvi ni shughuli muhimu ya kiuchumi katika Bahari ya Java. Kuna zaidi ya spishi 3,000 za viumbe vya baharini katika eneo hilo. Kuna pia hifadhi kadhaa za kitaifa kama Karimunjawa.

Eneo linalozunguka Bahari ya Java ni shabaha maarufu ya utalii. Wengi wanakuja kupiga mbizi na kupata picha za viumbe chini ya maji, mabaki ya meli zilizozama, matumbawe na sifongo.

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia yalitokea hapa mapigano ya baharini katika miezi ya Februari na Machi ya mwaka 1942 ambapo jeshi la majini la Japani lilishinda mataifa ya ushirikiano Uholanzi, Ufalme wa Muungano, Australia na Marekani yaliyojaribu kutetea Java.


Previous Page Next Page






Laôt Jawa ACE Javasee AF بحر جاوة Arabic Mar de Xava AST Yava dənizi AZ جاوه دنیزی AZB Ява диңгеҙе BA Segara Jawa BAN Яванскае мора BE Яванскае мора BE-X-OLD

Responsive image

Responsive image