John Calvin, kwa Kifaransa Jean Calvin au kizamani Jehan Cauvin (10 Julai 1509 - 27 Mei 1564) alikuwa mwanateolojia toka Ufaransa aliyeanzisha madhehebu maalumu ya Ukristo katika karne ya 16 akiunga mkono Matengenezo ya Kiprotestanti yaliyoanzishwa na Martin Luther nchini Ujerumani, lakini kwa kutofautiana naye katika mafundisho mbalimbali.
Mwalimu huyo aliandika kitabu akiweka mkazo kuelezea jinsi mapenzi ya Mungu yalivyokwishaamua juu ya maisha ya mwanadamu kabla ya huyo kuamua mwenyewe.