Irugwa ni kata ya Wilaya ya Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza, Tanzania.
Kata hiyo inaundwa na kisiwa cha Irugwa na visiwa vingine vidogo vya Kulazu, Buluza na Lyegoba.
Irugwa inavyo vijiji viwili: Sambi (yalipo makao makuu ya kata) na Nabweko. Kitongoji maarufu ni Buyanza (wenyewe wakijiita Washabunda) maana ndipo hasa zilipo huduma muhimu za jamii kama zahanati, ofisi ya kata, shule ya msingi na mitambo ya maji safi na maji taka bila kusahau mitambo ya kuzalisha umeme.
Kata ina shule za msingi tano ambazo ni Irugwa, Nabweko, Kulazu, Buluza na Lyegoba. Kuna shule ya sekondari moja iitwayo Irugwa.