Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Irugwa

Irugwa ni kata ya Wilaya ya Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza, Tanzania.

Kata hiyo inaundwa na kisiwa cha Irugwa na visiwa vingine vidogo vya Kulazu, Buluza na Lyegoba.

Irugwa inavyo vijiji viwili: Sambi (yalipo makao makuu ya kata) na Nabweko. Kitongoji maarufu ni Buyanza (wenyewe wakijiita Washabunda) maana ndipo hasa zilipo huduma muhimu za jamii kama zahanati, ofisi ya kata, shule ya msingi na mitambo ya maji safi na maji taka bila kusahau mitambo ya kuzalisha umeme.

Kata ina shule za msingi tano ambazo ni Irugwa, Nabweko, Kulazu, Buluza na Lyegoba. Kuna shule ya sekondari moja iitwayo Irugwa.


Previous Page Next Page






Irugwa CEB Irugwa Italian

Responsive image

Responsive image