Kafeini (kutoka Kiingereza caffeine) ni dutu ya alkaloidi katika mimea mbalimbali hasa mbuni na mchai. Inaathiri neva za mwanadamu ikiondoa uchovu na kuamsha ubongo.
Matumizi yake ni hasa katika vinywaji vya kahawa, chai na kinywaji cha mate ya Amerika Kusini, lakini pia katika madawa ya tiba na vinywaji nishati (energy drinks).