Kamerun ya Kijerumani ilikuwa koloni la Dola la Ujerumani kuanzia mwaka 1884 hadi 1916. Koloni hilo lilijumuisha maeneo ya Jamhuri ya Kamerun, pamoja na sehemu zilizopo sasa katika kaskazini mwa Gabon na Jamhuri ya Kongo, pia sehemu za magharibi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati na za kusini magharibi mwa Chad na maeneo mashariki mwa Nigeria.