Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Kanaani

Wakanaani walivyochorwa na Wamisri katika karne ya 13 KK.

Kanaani ni jina la zamani la eneo la Mashariki ya Kati ambalo siku hizi limegawanyika katika nchi za Israeli na Palestina, Lebanoni na sehemu za Magharibi za Jordan na Sirya.

Katika Biblia jina hilo (kwa Kiebrania כנען, knaʿn) linatumika zaidi kumaanisha sehemu ile tu ambayo ilitekwa na Waisraeli na kuitwa Israeli. Sehemu hiyohiyo baadaye tena ilikuja kuitwa pia Palestina, yaani nchi ya Wafilisti.

Baada ya mataifa hayo mawili kuteka sehemu kubwa upande wa Kusini kuanzia karne ya 13 KK, ile ya Kaskazini zaidi iliyobaki chini ya wakazi asili ilikuja kuitwa pia Foinike.

Katika eneo hilo kati ya Mesopotamia na Misri kuanzia milenia ya 4 KK ulistawi ustaarabu muhimu wa Kisemiti ambao, kati ya michango mingine, ni asili ya alfabeti.

Habari nyingi kuhusu ustaarabu huu zimejulikana hasa kwa njia ya akiolojia.


Previous Page Next Page






Kanaän AF Kanaan ALS ከነዓን (ጥንታዊ አገር) AM كنعانيون Arabic ܟܢܥܢ ARC كنعان ARZ Canán AST Kənan AZ Ханаан BE Ханаан BE-X-OLD

Responsive image

Responsive image