Kanisa la Kiorthodoksi la Eritrea ni madhehebu ya dini ya Ukristo iliyotawala makabila ya Eritrea kaskazini kwa karne kadhaa hadi sasa.
Wakristo hao wanaotaka kuzingatia imani sahihi ya Makanisa ya Kiorthodoksi ya Mashariki ni sehemu muhimu katika utamaduni wa Eritrea kama ulivyo kwa wenzao wa Ethiopia[1].
Kwa sasa lina waumini milioni 3.[2] wengi wao wakiishi nchini Eritrea,[3] lakini pia Ulaya na Amerika.