Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Karate

Mwanafunzi wa karate akiwa amevaa karategi.
Mashindano ya Karate
Kanda za karate zenye rangi mbalimbali
Mwalimu Hanashiro Chomo
Mashindano ya Karate duniani mnamo mwaka 2006 mjini Tampere, Finland, fainali ya uzani mzito kwa wanaume
Mashindano ya Karate duniani mnamo mwaka 2006 mjini Tampere, Finland, fainali ya uzani mzito kwa wanaume
Neno 'Karate' kwa maandishi ya kichina

Karate (pia kareti, kutoka Kijapani: 空手) ni aina ya michezo ya mapigano kutoka nchini Japani.[1] Ilianzishwa kwenye kisiwa cha Okinawa ikaenea Japani kwenye mwanzo wa karne ya 20 na kusambaa duniani baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia.[2]

Karate inatumia kama silaha za mapigano pande zote za mwili kama vile mkono, ngumi, kisugudi au mguu.

Mafunzo ya karate huwa na ngazi tatu:

  • kihon inahusu misingi
  • kata ni namna ya kutumia misingi hiyo
  • kumite ni matumizi yake katika mapigano

Kati ya michezo ya mapigano kama mchezo wa ngumi au kupiga mwereka karate inaweka mkazo kwa nguvu ya kiroho sawa na nguvu ya mwili.

Karate imefahamika duniani zaidi kutoka filamu za karate kuanzia miaka ya 1960.

Mwalimu wa karate kwa Kijapani huitwa "sensei" (kwa Kiingereza "master").

  1. Nussbaum, Louis-Frédéric. (2005). "Karate" in Japan Encyclopedia, p. 482.
  2. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2009-03-02. Iliwekwa mnamo 2009-03-02.

Previous Page Next Page






Karate AF Karate ALS Karate AN كاراتيه Arabic كاراطي ARY كاراتيه ARZ কাৰাটে AS Kárate AST Karate AZ کاراتئ AZB

Responsive image

Responsive image