Kiangazi (pia msimu au majira ya kiangazi) ni kipindi cha kila mwaka cha mvua kidogo, hasa katika tropiki. Hali ya hewa katika nchi za tropiki inatawaliwa na ukanda wa mvua wa kitropiki, ambao hutoka kaskazini hadi kusini mwa tropiki na kurudi katika kipindi cha mwaka. Nje ya tropiki, msimu wa joto ni kama kiangazi katika maeneo mengi. Msimu wa baridi pia unaweza kuhesabiwa kama msimu wa ukame kwa kusema kifiziolojia, kwa sababu hata ikiwa kuna mvua katika mfumo wa theluji, baridi hufanya mimea isiweze kufyonza maji kutoka udongo.