Kwa gari la kijeshi linalobeba silaha tazama hapa: Kifaru (jeshi)
Kifaru | ||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kifaru mweusi (Diceros bicornis)
| ||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||
| ||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||
Jenasi 4, spishi 5, nususpishi 16:
|
Vifaru au faru ni wanyamapori wakubwa wa familia Rhinocerotidae. Spishi mbili zinapatikana Afrika na nyingine tatu huko Asia. Nchini Uhindi wanabaki faru 2700 tu na hata faru weupe nao wameadimika sana duniani.
Faru hufahamika sana kwa umbo lake kubwa (ni miongoni mwa wanyama walanyasi wakubwa sana ambao wanabakia); huku kila spishi ya faru ikikaribia kuwa na uzito wa tani moja na ngozi ngumu ya kujilinda, yenye unene wa sentimeta 1.5 – 5.0; ubongo mdogo wa mamalia (gramu 400 – 600) na pembe kubwa. Hula sana majani.
Faru wana uwezo mkubwa wa kusikia na kunusa, lakini uoni wao si mzuri sana. Weusi huishi kwa miaka 60 na zaidi.
Faru huthaminiwa sana kutokana na pembe zao. Pembe hizo zimetengenezwa kwa keratini, protini, sawa na ile inayopatikana kwenye nywele na kucha.[1] Faru wa Afrika na wa Sumatra wana pembe mbili huku wale wa Uhindi na wa Java wakiwa na pembe moja tu. Faru wa Afrika hukosa meno ya mbele na kutegemea zaidi magego katika kusaga chakula.
{{cite web}}
: CS1 maint: date auto-translated (link)