Kitabu cha Sefania ni kimojawapo kati ya vitabu vya Tanakh (yaani Biblia ya Kiebrania), hivyo kinapatikana pia katika Agano la Kale ambalo ni sehemu ya kwanza ya Biblia ya Kikristo.
Kutokana na ufupi wake kimepangwa tangu kale kati ya vitabu 12 vya Manabii Wadogo.