Majira ya mvua (pia: msimu wa mvua) ni kipindi cha kila mwaka cha mvua nyingi, hasa katika tropiki. Hali ya hewa katika nchi za tropiki inatawaliwa na ukanda wa mvua wa kitropiki, ambao hutoka kaskazini hadi kusini mwa tropiki na kurudi katika kipindi cha mwaka mmoja. Nje ya tropiki, majira ya mvua yanaweza kuwa wakati wa majira ya joto au ya baridi kulingana na tabianchi ya eneo husika.