Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Mama Teresa

Mama Teresa mnamo mwaka 1990.

Mama Teresa wa Kolkata (26 Agosti 19105 Septemba 1997) alikuwa bikira wa Kanisa Katoliki aliyejulikana kimataifa hasa kutokana na huduma zake kwa watu maskini katika mji wa Kolkata (Uhindi) na kwingineko iliyofanya apatiwe tuzo ya Nobel ya Amani mwaka 1979.

Upendo wake usio na mipaka kwa ndugu maskini zaidi ulikusudiwa naye kuzima kiu ya Kristo aliyeachika msalabani.

Kwa mwongozo wake kupitia njozi alianzisha shirika la Masista Wamisionari wa Upendo halafu taasisi nyingine zenye lengo la kujitosa kikamilifu kuhudumia wagonjwa na wasio na chochote[1].

Tarehe 19 Oktoba 2003 alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa mwenye heri. Baada ya muujiza wa pili kufanywa na Mungu kwa maombezi yake, Papa Fransisko amemtangaza kuwa mtakatifu tarehe 4 Septemba 2016.

Sikukuu yake huadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Septemba[2]. Siku hiyohiyo imetangazwa na mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa kuwa siku ya kimataifa ya upendo kuanzia mwaka 2013.

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/90013
  2. Martyrologium Romanum

Previous Page Next Page






Moeder Teresa AF Mutter Teresa ALS እምዬ ቴሬሳ AM Santa Teresa de Calcuta AN الأم تريزا Arabic الام تيريزا ARZ মাদাৰ টেৰেছা AS Teresa de Calcuta AST Tayka Teresa AY Tereza Ana AZ

Responsive image

Responsive image