Wilaya ya Mbarali ni wilaya mojawapo kati ya 7 za Mkoa wa Mbeya. Wilaya hiyo ilianzishwa mnamo mwaka 2000.
Upande wa Kaskazini Mashariki inapakana na Wilaya ya Iringa Vijijini, upande wa Mashariki inapakana na Wilaya ya Njombe, upande wa Kusini inapakana na wilaya ya Mbeya na Kaskazini na Wilaya ya Chunya.