Mkoa wa Pwani ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 61000.
Mkoa umepakana upande wa Kaskazini na Tanga, upande wa mashariki na Dar-es-Salaam na Bahari Hindi, upande wa kusini na mkoa wa Lindi na upande wa magharibi na mkoa wa Morogoro.
Makao makuu ya mkoa yako Kibaha.