Mumia (kutoka Kiarabu مومياء mumia; pia: mumiani; kwa Kiingereza: mummy) ni maiti wa binadamu au mzoga wa mnyama iliyokauka bila kuoza. Hali hiyo inaweza kutokea kiasili katika mazingira maalumu au kwa kutumia mbinu fulani. Mchakato wa kuoza huzuiwa na baridi kali, katika mazingira yabisi (pasipo na unyevu hewani) na mwendo wa hewa, kwa kukosa oksijeni au kwa kutumia kemikali fulani.