Muungo kemia (kwa Kiingereza: chemical bond) ni kani inayoshikiza atomu, ioni na molekuli na hivyo kuwa msingi wa kutokea kwa kampaundi.
Kani hiyo inaweza kutokana na kani umemetuamo (electrostatic force) katika muungo ionia au na muungo kovalensi ambapo atomu zinashirikiana elektroni.