Oaxaca ([wɑˈhɑkə]; jina rasmi: Estado Libre y Soberano de Oaxaca; Kiswahili: dola huru na enzi ya Oaxaca) ni moja kati ya majimbo ya Mexiko upande wa jusini ya nchi, magharibi wa shingo ya nchi ya Tehuantepec. Mji mkuu na mji mkubwa ni Oaxaca. Imepakana na Guerrero, Puebla, Veracruz na Chiapas. Upande wa kusini ni maji ya Pasifiki.
Kunako mwaka wa 2005, idadi ya wakazi ilikuwa 3,506,821. Una eneo la 93,952 km².
Oaxaca ilikuwa sehemu ya maeneo ya Wazapotec na Wamixtec. Jina lake limetokana na jina la mji wa Oaxaca.
Gavana wa jimbo ni Ulises Ruiz Ortiz.
Lugha rasmi ni Kihispania.