Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Pango la Noeli

Pango la Greccio lilivyochorwa na Giotto, 1290-1295 hivi, katika Basilika la Mt. Fransisko, Assisi, Italia.
Picha ya zamani ya Mt. Fransisko iliyotunzwa katika konventi ya Greccio.
Pango la Piazza di Spagna mjini Roma.

Pango la Noeli (au pango) ni sanaa inayoonyesha jinsi Yesu Kristo alivyozaliwa.

Hiyo ni kadiri ya desturi za Karne za Kati, ambazo asili yake ni Fransisko wa Asizi (1182-1226).

Ndiye aliyeandaa pango hai akitumia watu na wanyama hai ili yeye na watu wa Greccio wajisikie zaidi washiriki wa tukio la usiku wa Noeli (1223).

Kabla yake picha na sanamu za uzazi wa Yesu zilikuwa zinahusu zaidi maadhimisho ya liturujia kuliko uhalisia wa tukio la Bethlehemu.

Kumbe Fransisko, aliyewahi kuhiji katika Nchi takatifu ya Israeli, alipenda hata wasiofika huko waelewe zaidi hali ilivyokuwa.


Previous Page Next Page






مغارة الميلاد Arabic مغارة الميلاد ARZ Belen BCL Шопка BE Kraou Nedeleg BR Pessebre Catalan Jesličky Czech Julekrybbe Danish Weihnachtskrippe German Φάτνη της Γεννήσεως Greek

Responsive image

Responsive image