Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Panzi-bahari

Panzi-bahari
Panzi-bahari wa Mediteranea (Cheilopogon heterurus)
Panzi-bahari wa Mediteranea (Cheilopogon heterurus)
Panzi-bahari akianza kuruka
Panzi-bahari akianza kuruka
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Actinopterygii (Samaki walio na mapezi yenye tindi)
Oda: Beloniformes (Samaki kama ngarara)
Familia: Exocoetidae (Samaki walio na mnasaba na panzi-bahari)
Risso, 1827
Ngazi za chini

Jenasi 7 na spishi 64, 27 katika Afrika:

Panzi-bahari, panzi-maji, panzimai au ndegemaji ni samaki wa baharini wa familia Exocoetidae katika oda Beloniformes ambao wanaweza kuruka juu ya maji na kwenda mbali kiasi, mpaka mamia ya mita. “Mabawa” yao ni mapeziubavu kwa kweli. Katika spishi za jenasi Cheilopogon na Cypselurus hata mapezitumbo yanatumika kama mabawa na kwa hivyo huitwa “panzi-bahari mabawa-manne”. Uwezo huu usio wa kawaida katika samaki ni utaratibu wa asili wa utetezi kuepuka mbuai. Pengine pezimgongo ni refu na huitwa tanga.

Samaki wa familia Triglidae huitwa panzi-bahari pia.


Previous Page Next Page