Panzi-bahari | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Panzi-bahari wa Mediteranea (Cheilopogon heterurus)
Panzi-bahari akianza kuruka
| ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Jenasi 7 na spishi 64, 27 katika Afrika:
|
Panzi-bahari, panzi-maji, panzimai au ndegemaji ni samaki wa baharini wa familia Exocoetidae katika oda Beloniformes ambao wanaweza kuruka juu ya maji na kwenda mbali kiasi, mpaka mamia ya mita. “Mabawa” yao ni mapeziubavu kwa kweli. Katika spishi za jenasi Cheilopogon na Cypselurus hata mapezitumbo yanatumika kama mabawa na kwa hivyo huitwa “panzi-bahari mabawa-manne”. Uwezo huu usio wa kawaida katika samaki ni utaratibu wa asili wa utetezi kuepuka mbuai. Pengine pezimgongo ni refu na huitwa tanga.
Samaki wa familia Triglidae huitwa panzi-bahari pia.