Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Papa Damaso I

Papa Damaso I.

Papa Damaso I (takriban 30411 Desemba 384) alikuwa Papa kuanzia tarehe 1 Oktoba 366 hadi kifo chake[1]. Alitokea Roma, Italia. Jina lake la kuzaliwa pia lilikuwa Damasus.

Alimfuata Papa Liberius akafuatwa na Papa Siricius.

Kati ya magumu ya nyakati zake, aliitisha sinodi mbalimbali ili kutetea imani ya Mtaguso wa kwanza wa Nisea dhidi ya mafarakano na uzushi.

Pia alimuagiza Jeromu kutafsiri katika Kilatini vitabu vitakatifu vya Biblia ya Kikristo, naye mwenyewe aliheshimu makaburi ya wafiadini kwa kuyapamba kwa mashairi [2].

Mchango wake mkubwa zaidi ni kuthibitisha kanuni ya Biblia kama ilivyo hadi leo katika Kanisa Katoliki.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni 11 Desemba.[3].

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.html/ index.html#holy-father
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/30350
  3. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Previous Page Next Page