Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Spitsbergen

Mahali pa Spitsbergen
Spitzbergen kutoka satelaiti wakati wa joto (mwezi wa Julai: peupe ni barafu)

Spitsbergen (pia: Spitzbergen) ni kisiwa kikubwa cha funguvisiwa la Svalbard linaloitwa mara nyingi kwa jina la Spitsbergen vilevile kwa jumla. Kiko ndani ya Bahari ya Aktiki na eneo lake ni km² 39,044. Funguvisiwa lote ni sehemu ya ufalme wa Norwei.

Mwinuko mkuu ni mlima wa Newtontoppen wenye kimo cha mita 1717.

Wakazi wa kisiwa ni Wanorwei na Warusi: kwa jumla hawazidi watu 2100.

Biashara ya kisiwa ni utalii na migodi pekee; hakuna kilimo kutokana na baridi. Mimea hustawi katika wiki chache za joto kidogo na hii inatokea kwenye asilimia 10 ya eneo la kisiwa pekee, maeneo mengine ni baridi mno.

Kuna kijiji kimoja ambacho ni Longyearbyen wenye wakazi 1700. Cha pili ni Barentszburg kinachokaliwa na Warusi 400 wanaozidi kupungua. Pyramiden ilikuwa kituo kikubwa cha kuchimba makaa lakini haina watu tena tangu mwaka 2000.


Previous Page Next Page