Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Ukeketaji

map
Kiwango cha ukeketaji duniani: Afrika inaongoza pamoja na Yemen na Kurdistan ya Iraq.

Ukeketaji (pia: tohara ya mwanamke; kwa Kiingereza: female circumcision, female genital mutilation; kifupi: FGM) ni tendo la kukata sehemu za nje za viungo vya uzazi vya mwanamke.

Neno linalotokana na mzizi keket, ambao unabeba maana ya kuharibu.

Mara nyingi tendo la ukeketaji linaitwa pia "tohara" kwa kulifananisha na upasuaji mdogo wa wanaume, lakini mambo ni tofauti kabisa.

Hapa sehemu za nje za viungo vya uzazi zinakatwa kusudi wasifurahie sana tendo la ndoa, hivyo wawe waaminifu zaidi kwa waume wao.

Ukeketaji umeenea hasa kati ya mataifa na makabila wenye asili ya bonde la Naili na majirani wao.

Kinyume na tohara ya wavulana matabibu wanaona hasara nyingi katika desturi hiyo. Ukeketaji unasababisha wasichana wengi kufa na wengine wengi kupatwa na maumivu makali wakati wa hedhi, wa tendo la ndoa na wa kujifungua.

Kwa sababu hizo serikali nyingi za dunia zimeupiga marufuku.

Pia madhehebu kadhaa yanatoa mafundisho kuwa ni kinyume cha masharti ya dini yao.

Juhudi zimefanikiwa kwa kiasi fulani katika baadhi ya nchi.

Kiwango kikubwa sana Kiwango kikubwa Kiwango cha wastani Kiwango cha chini Kiwango cha chini sana
Somalia
98%
Gambia
76%
Guinea-Bissau
50%
Jamhuri ya Afrika ya Kati
24%
Iraq
8%
Guinea
96%
Burkina Faso
76%
Chad
44%
Yemen
23%
Ghana
4%
Jibuti
93%
Ethiopia
74%
Côte d'Ivoire
38%
Tanzania
15%
Togo
4%
Egypt
91%
Mauritania
69%
Kenya
27%
Benin
13%
Niger
2%
Eritrea
89%
Liberia
66%
Nigeria
27%
Cameroon
1%
Mali
89%
Senegal
26%
Uganda
1%
Sierra Leone
88%
Sudan
88%

Previous Page Next Page