Ukuta mkubwa wa China ni kati ya majengo makubwa kabisa yaliyowahi kujengwa duniani. Ni mfululizo wa kuta na ngome unaofuata mpaka kati ya China na mbuga baridi za Asia ya Kaskazini na Asia ya Kati. Ulijengwa kwa shabaha ya kulinda China dhidi ya mashambulio ya makabila ya wahamiaji wa sehemu hizo.
Jumla ya kuta zote ina urefu wa kilomita zaidi ya 21,000. [1][2]
Ujenzi ulianza katika karne ya 7 KK na kuendelea hadi karne ya 16 BK.[3]