Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Umisionari

Umisionari ni utendaji unaolenga kueneza dini fulani, hasa zile zinazokusudiwa kuwa za kimataifa kutokana na misingi ya imani yake, kwamba ndivyo Mungu anavyotaka na alivyoagiza.

Asili ya neno hilo ni missio (kwa Kilatini utume).

Mmisionari au mwanamisheni ndiye mtu anayefanya kazi hiyo, hasa katika maeneo ambayo dini hiyo haipo au haijakua.

Mara nyingi wamisionari wanachangia pia maendeleo ya jamii, hasa kupitia elimu, utabibu, utunzaji wa watoto yatima na walioathiriwa na vita na maradhi mbalimbali.

Pengine uenezaji wa dini unatumia mbinu zisizokubalika kijamii, kama vile kulazimisha kwa namna moja au nyingine mtu asiyetumwa na moyo wake kukubali dini mpya.


Previous Page Next Page






Празелітызм BE Прозелитизъм Bulgarian Proselitisme Catalan Proselytismus Czech Proselytiaeth CY Proselytismus German Προσηλυτισμός Greek Proselytism English Prozelitismo EO Proselitismo Spanish

Responsive image

Responsive image