Kata ya Utengule/Usongwe | |
Mahali pa Utengule Usongwe katika Tanzania |
|
Majiranukta: 8°40′47″S 33°51′35″E / 8.67972°S 33.85972°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Mkoa | Mbeya |
Wilaya | Mbeya Vijijini |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 55,082 |
Utengule/Usongwe ni kata ya Wilaya ya Mbeya Vijijini katika Mkoa wa Mbeya, Tanzania. Kijiji cha Utengule kiko kilomita 16 kutoka Mbeya mjini kupitia Mbalizi.
Katika sensa iliyofanyika mwaka 2022 wakazi walihesabika kuwa 55,082 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 41,952 [2] walioishi humo. Msimbo wa posta ni 53208.
Mazingira ya Utengule pana mashamba ya kahawa na shamba kubwa ambalo ni mali ya Waswisi walioanzisha pia hoteli ya Utengule Country Club. Kuna kanisa na chuo cha Biblia cha Moravian.