Wagweno ni kabila la watu wenye asili ya Kenya wanaoishi Tanzania katika Mkoa wa Kilimanjaro, upande wa Kaskazini wa Milima ya Ugweno.
Lugha yao ni Kigweno. Utamaduni wao ni mchanganyiko wa tamaduni za Kipare na Kichaga. Wagweno wanajishughulisha na kilimo na ufugaji. Wanalima ndizi, mahindi, kahawa na maharage. Pia Ugweno kuna kilimo cha matunda kama parachichi, maembe na mapensheni.
Shughuli za ufugaji zinahusisha ufugaji wa ng'ombe, mbuzi na kondoo.