Wakamba ni kabila la watu wa Kenya wakikalia eneo la Ukambani kati ya Nairobi, Voi na kati ya mlima Kenya na mlima Kilimanjaro. Wakamba ni kabila kubwa la nne nchini Kenya.
Hutumia lugha ya Kikamba ambacho ni lugha ya Kibantu karibu na Kigikuyu, Kiembu na Kimeru.