Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Wameru (Tanzania)

Kabila la Wameru huishi pembezoni mwa mlima Meru.

Wameru wa Tanzania (au "Warwa") ni kabila la watu wa Kibantu wa jamii ya Wachaga wanaoishi hasa kwenye Mlima Meru katika Mkoa wa Arusha, kaskazini mwa nchi ya Tanzania.

Lugha yao ni Kirwa[1].

Wanakadiriwa kuwa milioni 2, wengi wao wakifuata dini ya Ukristo.

Mbali na jina, Wameru hao ni tofauti kabisa na Wameru wa Kenya kwa historia na utambulisho. Sanasana ni kwamba pande zote mbili ni wakulima wenye bidii kubwa[2].

Inasemekana Wameru walifikia mlima huo miaka 800 hivi iliyopita wakitokea milima ya Usambara, Mkoa wa Tanga. Walikuta huko wawindaji walioitwa Wakoningo ambao walikuja kumezwa na jamii ya Wameru.[3]

  1. [1]
  2. Fosbrooke, Henry. "waMeru People". Arusha Integrated Regional Development Plan. uk. 5. Iliwekwa mnamo 2016-09-17.
  3. "HISTORIA YA WAMERU". ONLINE TUITION. Iliwekwa mnamo 2024-01-13.

Previous Page Next Page






Ουαμέρου Greek Wameru English

Responsive image

Responsive image