Wasiosadiki Utatu ni Wakristo ambao wanakusha fundisho hilo la msingi la madhehebu karibu yote ya dini iliyoanzishwa na Yesu.
Biblia haitumii neno Utatu, ambalo limetungwa na wanateolojia katika jitihada za kufafanua ukweli wa Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu na wa Roho Mtakatifu.
Kwa kuwatambua wote wawili kuwa wa milele lakini si Baba, wanateolojia wengi, hasa mababu wa Kanisa, walikiri kuwa zote tatu ni nafsi tofauti za Mungu pekee.
Mitaguso ya kiekumene kuanzia karne ya 4 ilithibitisha mafundisho hayo kama imani sahihi na kutupilia mbali yaliyo kinyume kama uzushi.[1][2][3][4]
Hata hivyo Waario na wengineo hawakukubali dogma hizo,[5] hivyo asilimia ndogo ya Wakristo imeendelea kukataa kusadiki fumbo la Utatu, na kukiri umoja wa nafsi ya Mungu,[6][7][8][9] ingawa kwa kutofautiana wao kwa wao.[10]
Kati ya makundi makubwa zaidi yenye msimamo huo kuna Wamormoni na Mashahidi wa Yehova, lakini pia baadhi ya Wapentekoste.
[In the 2nd century,] Jesus was either regarded as the man whom God hath chosen, in whom the Deity or the Spirit of God dwelt, and who, after being tested, was adopted by God and invested with dominion, (Adoptionist Christology); or Jesus was regarded as a heavenly spiritual being (the highest after God) who took flesh, and again returned to heaven after the completion of his work on earth (pneumatic Christology)