Wavuti wa Walimwengu (kifupi: WWW; pia: Wavuti; Kiingereza: World Wide Web), ni sehemu ya tovuti yenye wavuti nyingi. Sehemu nyingine za tovuti, kama huduma ya baruapepe (email) si sehemu ya WWW.
Tovuti za WWW zinafanywa na kurasa zenye matinikivo (hypertext) zinazoelekezana kwa njia ya viungokivo (hyperlinks). Yaliyomo ya wavuti hizo ni mara nyingi matini (text) pamoja na picha za mgando na za video, hati za sauti au muziki.
Kati ya lugha za mantikikivo zinazotumiwa zaidi ni HTML.