Wawanji ni kabila kutoka wilaya ya Makete, katika milima ya Kipengere ya Mkoa wa Njombe, sehemu ya kusini ya nchi Tanzania. Asilimia kubwa ya Wawanji wapo sehemu za Ikuwo na Matamba, maarufu kama bonde la Uwanji.
Mwaka 2003 idadi ya Wawanji ilikadiriwa kuwa 28,000[1]. Lugha yao ni Kiwanji yenye misamiati ambukizi toka makabila jirani.
Wawanji ni majirani kabisa wa kabila la Wakinga, wakipakanishwa na hifadhi ya Kitulo.