Addis Ababa

Jiji la Addis Ababa
Jiji la Addis Ababa
Jiji la Addis Ababa is located in Ethiopia
Jiji la Addis Ababa
Jiji la Addis Ababa

Mahali pa mji wa Addis Ababa katika Ethiopia

Majiranukta: 9°1′48″N 38°44′24″E / 9.03000°N 38.74000°E / 9.03000; 38.74000
Nchi Ethiopia
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 3,352,000
Tovuti:  www.addisababacity.gov.et
Ramani ya Ethiopia ikionyesha Addis Ababa ilipo.
Addis Ababa, inavyoonekana kutoka angani.
Zaidi ya asilimia 51 ni wanawake.

Addis Ababa (pia Addis Abeba; kwa Kiamhara አዲስ አበባ, "Ua Jipya"; kwa Kioromo Finfinne) ni mji mkuu wa Ethiopia na wa Umoja wa Afrika.

Ina hadhi ya mji wa kujitawala (ras gez astedader) kama jimbo la Ethiopia.

Mji wenyewe una watu kutoka makabila 80, wakiongea lugha 80, na jamii za Waislamu na Wakristo.

Addis Ababa iko mita 2,500 juu ya usawa wa bahari kwa 9.03° N 38.74° E). [1]

Mwaka 2016, idadi ya wakazi ilikuwa 3,352,000 [2], na kwa hiyo Addis Ababa ndio mji mkubwa nchini.

Eneo hii lilichaguliwa na Malkia Taytu Betul na mji kuanzishwa mwaka wa 1886 na mume wake, Mfalme Menelik II, na sasa mji huu una umma milioni nne, na asilimia nane ya ukuzi wa uchumi.

Mji huu uko kwenye Mlima Entoto na ni makazi maalum ya Chuo Kikuu cha Addis Ababa. Chuo Kikuu cha Addis Ababa kilijulikana kama Chuo Kikuu cha Haile Selassie I, kutokana na jina la Mfalme wa mwisho wa Ethiopia, ambaye alitoa jumba la mfalme (Jumba Guenete Leul) liwe makao maalum ya Chuo Kikuu cha Addis Ababa mwaka wa 1961.

  1. "World-Gazeteer". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2011-03-25. Iliwekwa mnamo 2006-05-14.
  2. "World-Gazeteer". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2007-10-01. Iliwekwa mnamo 2006-05-14.

Addis Ababa

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne