Bombomu

Bunduki ya Gatling ilikuwa bombomu ya kwanza
Vickers machine gun calibre .303 ilikuwa modeli iliyopendwa kabla ya Vita Kuu I
Bombomu M2 na maganda matupu ya ramia
Askari wa Uganda na bombomu
Bombomu nzito kwenye manowari
Hii ni PKM Machine Gun.

Bombomu (au: bunduki ya mtombo; bunduki ya rashasha; kwa Kiingereza Machine gun) ni silaha ya moto kubwa kiasi inayofyatulia haraka risasi nyingi za mfululizo kutoka kwenye mkanda wa risasi muda wote kiwashio cha silaha inashikwa hadi akiba ya ramia imekwisha, kwa kawaida kwa kiwango cha raundi 300 kwa dakika au zaidi.

Akiba ya ramia imo ama katika chemba yake au ramia zimepangwa katika ukanda unaopita kwenye bombomu. Bombomu ndogu hubebwa na askari mmoja lakini modeli nzito kiasi huhitaji watu wawili hadi watatu.

Bombomu ndogo zaidi huitwa bunduki ya nusu mtombo, hutumiwa kama silaha ya kawaida ya askari, lakini hutumia ramia za bastola. Ni nyepesi, hailengi mbali sana na kusudi lake ni pigano dhidi ya adui aliye karibu.

Bombomu kubwa zaidi hubebwa tena wa watu, hufungwa juu ya gari au magurudumu huitwa mzinga wa bombomu. Hutumiwa pia kwenye manowari na boti za kijeshi, halafu kwenye ndege za kijeshi.

Tofauti na hizo, bunduki za shambulio, silaha za risasi, bastola au vidogo vinaweza kuwa na uwezo wa moto wa moja kwa moja, lakini si kwa ajili ya moto unaoendelea.

Kama darasa la bunduki za haraka za kijeshi, bunduki za silaha ni silaha za moja kwa moja zilizopangwa kutumiwa kama silaha za usaidizi na zinazotumiwa kwa ujumla wakati zilizounganishwa na mlima-au kufukuzwa kutoka chini kwenye bipod au safari.


Bombomu

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne