Carl Linnaeus (tamka: Karl Lineus; pia kwa umbo la Kilatini Carolus Linnaeus na baadaye Carl von Linné; 23 Mei 1707 – 10 Januari 1778) alikuwa mwanasayansi nchini Uswidi aliyeweka misingi ya biolojia ya kisasa kwa kuunda utaratibu wa taksonomia au uainishaji wa mimea na wanyama katika vikundi mbalimbali na kuvipa majina ya kisayansi.