David Livingstone (19 Machi 1813 – 4 Mei 1873) alikuwa mmisionari na mpelelezi kutoka Uskoti katika Afrika ya kusini na kati.
Alijulikana kwa jitihada zake za kupambana na biashara ya watumwa na safari za kati ya Afrika ya Kusini na Tanganyika hadi Kongo.