Guinea ni jina la kihistoria kwa ajili ya kanda ya kusini ya Afrika ya Magharibi kati ya jangwa Sahara na Atlantiki. Nchi zote kuanzia Senegal hadi kaskazini ya Angola zilihesabiwa kuwa "Guinea". Waandishi wa Ulaya walitofautisha "Guinea ya Juu" (Senegal hadi Kamerun) na "Guinea ya Chini" (Kamerun hadi Angola).