Helgoland ni fungukisiwa ndogo cha Kijerumani katika Bahari ya Kaskazini takriban 70 km mbele ya Ujerumani bara. Ina visiwa viwili: Helgoland yenyewe ni kisiwa kinachokaliwa na watu halafu kisiwa kisicho na watu cha "Düne" (= tuta la mchanga). Kisiwa kikuu kina urefu wa 1700 m na wakazi 1,650.
Kiutamaduni Helgoland ni sehemu ya Frisia; wenyeji wanasema Kifrisia na Kijerumani. Iliwahi kuwa sehemu za nchi za Denmark na Ujerumani na kwa muda wa karne ya 19 BK pia chini ya Uingereza.
Zamani wakazi wa Helgoland walikuwa wavuwi na mabaharia. Tangu karne ya 19 utalii ilianza kuwa muhimu siku hizi wengi wanajipatia maisha kwa njia ya utalii.