Hifadhi ya Ziwa Manyara

Swala kwenye Ziwa Manyara.

Hifadhi ya Ziwa Manyara ni hifadhi ya Taifa ya Tanzania iliyo maarufu sana nchini kwa simba wanaopanda juu ya miti. Aina hii ya simba hupatikana ndani ya hifadhi hii pekee barani Afrika.

Hifadhi hii iko umbali wa kilometa 126 kutoka Arusha mjini ina ukubwa wa kilometa za mraba 325 hivi.

Hifadhi hiyo iko katika Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Manyara, lakini mikoa hiyo miwili ya utawala haina mamlaka juu ya hifadhi, bali inasimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Taifa ya Tanzania.

Jina la hifadhi hii limetokana na mmea wa mnyaa ambao katika lugha ya Kimasai hujulikana kama Elmanyarai na sehemu kubwa ya hifadhi hii ni ziwa Manyara.


Hifadhi ya Ziwa Manyara

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne