Kifua kikuu

mapafu yanayoonyesha maambukizi ya Kifua kikuu
Kifua Kikuu
Mwainisho na taarifa za nje
Kundi MaalumuInfectious diseases, pulmonology Edit this on Wikidata
ICD-10A15.A19.
ICD-9010018
OMIM607948
DiseasesDB8515
MedlinePlus000077 Kigezo:MedlinePlus2
eMedicinemed/2324
MeSHD014376

Kifua kikuu (kwa Kiingereza tuberculosis, kifupi TB) ni ugonjwa wa kuambukizwa ulio hatari. Ugonjwa huu husababishwa na aina mbalimbali za bakteria ambazo hujulikana kama Mycobacterium tuberculosis.[1]

Kifua kikuu kwa kawaida kinaathiri mapafu, lakini pia kinaweza kuathiri sehemu nyingine za mwili.

Kifua kikuu husambazwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kwa kupitia hewa wakati anapokohoa, kupiga chafya, au mate yake yakiwa hewani[2]

Maambukizi mengi hayana dalili wala hayaleti madhara. Lakini moja kati ya maambukizo kumi yasiyoleta madhara hatimaye huendelea na kuwa ugonjwa kamili. Kama kifua kikuu kisipotibiwa, kinaua zaidi ya 50% ya watu walioambukizwa.

Dalili za kawaida za maambukizi ya kifua kikuu kinacholeta madhara ni kikohozi sugu na kukohoa damu, Kohozi, homa, kutokwa na jasho usiku, na kukonda. Maambukizi ya viungo vingine husababisha dalili mbalimbali. Njia ya kitaalamu ya utambuzi wa kifua kikuu kwa kutumia eksirei ya kuchunguza ugonjwa hujulikana kama eksirei ya kifua na pia wanatumia hadubini na kufanya uchunguzi wa vimelea maradhi vya majimaji ya mwilini. Uchunguzi wa kifua kikuu kisicholeta madhara hutumia kipimo kiitwacho kipimo cha ngozi (TST) na vipimo vya damu.

tiba si rahisi na inabidi kupewa dawa nyingi za kinga mwili kwa kipindi kirefu. Mawasiliano ya kijamii pia yanapimwa na kutibiwa kama inavyotakiwa. Dawa zinazoshindwa kutibu magonjwa ni tatizo kubwa la maambukizi sugu mengi ya kifua kikuu]] (MDR-TB).

Ili kuzuia kifua kikuu, ni lazima watu wapimwe ugonjwa na wapate chanjo ya bacillus Calmette - Guérin.

Wataalamu wanaamini kwamba theluthi moja ya idadi ya watu duniani waliambukizwa kifua kikuu,[3] na kila sekunde kuna mtu ambaye anaambukizwa [3]. Mwaka 2007, kadri ya watu 13,700,000 duniani waliambukizwa kifua kikuu kinacholeta madhara sugu. Mwaka 2010, kadri ya milioni 8.8 ya watu waliambukizwa na milioni 1.5 ya watu walifariki baada ya kuambukizwa na kifua kikuu, na wagonjwa wengi wanapatikana katika nchi zinazoendelea.[4] Idadi halisi ya wagonjwa wa kifua kikuu imekuwa ikipungua tangu mwaka 2006, na kesi mpya zimeshuka tangu mwaka 2002.[4]

Kifua kikuu si ugonjwa unaosambazwa sawasawa duniani kote. Kadri ya 80% ya watu katika nchi nyingi za Asia na Afrika waliofanyiwa kipimo cha ngozi walionekana wameambukizwa, lakini ni asilimia 5-10% tu ya wananchi wa Marekani ambao walionekana na ugonjwa huo.[1] Watu wengi waliopo katika nchi zilizoendelea wanaambukizwa kifua kikuu kwa sababu ya kutokuwa na kinga. Kwa kawaida, hawa watu wanaambukizwa kifua kikuu baada ya kuambukizwa na VVU na hatimaye wanapatwa na UKIMWI.[5]

  1. 1.0 1.1 Kumar V, Abbas AK, Fausto N, Mitchell RN (2007). Robbins Basic Pathology (tol. la 8th). Saunders Elsevier. ku. 516–522. ISBN 978-1-4160-2973-1.{{cite book}}: CS1 maint: multiple names: authors list (link)
  2. Konstantinos A (2010). "Testing for tuberculosis". Australian Prescriber. 33 (1): 12–18.
  3. 3.0 3.1 "Tuberculosis Fact sheet N°104". World Health Organization. Novemba 2010. Iliwekwa mnamo 26 Julai 2011.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. 4.0 4.1 World Health Organization (2011). "The sixteenth global report on tuberculosis" (PDF).
  5. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named Lancet11

Kifua kikuu

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne