Léopold Sédar Senghor | |
![]() | |
Rais wa kwanza wa Senegal
| |
Muda wa Utawala 6 Septemba 1960 – 31 Disemba 1980 | |
Waziri Mkuu | Abdou Diouf |
---|---|
mtangulizi | Office created |
aliyemfuata | Abdou Diouf |
tarehe ya kuzaliwa | Joal, Afrika ya Magharibi ya Kifaransa (leo Senegal) | 9 Oktoba 1906
tarehe ya kufa | 20 Desemba 2001 (umri 95) Verson, Ufaransa |
chama | Chama cha Kisoshalisti cha Senegal |
ndoa | Ginette Éboué (1946-1956) Colette Hubert Senghor (m. 1957–2001);hadi kifo |
mhitimu wa | Chuo Kikuu cha Paris |
dini | Kanisa Katoliki |
signature | ![]() |
Léopold Sédar Senghor (9 Oktoba 1906 – 20 Desemba 2001) alikuwa mshairi, mwanasiasa na hatimaye rais wa kwanza wa Senegal kati ya miaka 1960 na 1980.
Senghor alikuwa Mwafrika wa kwanza aliyechaguliwa kuwa mwanachama wa Académie française. Kabla ya uhuru wa nchi yake aliunda chama cha Umoja wa Kidemokrasia wa Senegal (kwa Kifaransa: Bloc démocratique sénégalais; kwa Kiingereza: Senegalese Democratic Bloc). Wengi wanamhesabu kati ya wataalamu Waafrika muhimu zaidi katika karne ya 20.