Maria Curie (jina kamili: Maria Salomea Skłodowska-Curie; 7 Novemba 1867 – 4 Julai 1934) alikuwa mwanafizikia na mwanakemia Mpolandi na Mfaransa aliyepata Tuzo ya Nobel ya Fizikia mwaka 1903 na Tuzo ya Nobel ya Kemia mwaka 1911. Marie Curie ni binadamu pekee aliyepokea tuzo ya Nobel kwa sayansi mbili tofauti.