Mapatano baina Uingereza na Ujerumani kuhusu Afrika na Helgoland (kifupi mkataba wa Helgoland-Zanzibar) yalifanywa kati ya Ujerumani na Uingereza tarehe 1 Julai 1890. Pande zote mbili zilielewana juu ya mipaka ya makoloni yao au maeneo walimotaka kuwa na athira kuu katika Afrika.
Mkataba ulihusu maeneo katika Afrika ya Mashariki, Afrika ya Kusini-Magharibi (leo Namibia) na Afrika ya Magharibi (Togo ya leo) pamoja na kisiwa cha Helgoland mbele ya pwani ya Ujerumani katika Bahari ya Kaskazini.