Mkoa wa Rukwa |
|
Mahali pa Mkoa wa Rukwa katika Tanzania | |
Majiranukta: 7°0′S 31°30′E / 7.000°S 31.500°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Wilaya | 4 |
Mji mkuu | Sumbawanga |
Serikali | |
- Mkuu wa Mkoa | Joachim Wangabo |
Eneo | |
- Jumla | 22,792 km² |
Idadi ya wakazi (2022) | |
- Wakazi kwa ujumla | 1,540,519 |
Tovuti: http://www.rukwa.go.tz/ |
Mkoa wa Rukwa ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 55000.
Unapakana na mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi upande wa kaskazini, mkoa wa Mbeya upande wa mashariki, Zambia kusini na upande wa magharibi Ziwa Tanganyika lililo mpaka na Kongo pia.
Makao makuu ya mkoa ni Sumbawanga.
Kabla ya kumegwa mwaka 2012 eneo la mkoa lilikuwa takriban km² 70,000. Kwa sasa lina kilomita ya mraba 22,792.
Kusini mwa mkoa liko ziwa Rukwa ambalo ni kati ya maziwa makubwa ya Afrika ya Mashariki.