Morisi

Republic of Mauritius
République de Maurice
Bendera ya Mauritius Nembo ya Mauritius
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Stella Clavisque Maris Indici
(Kilatini: Nyota na ufunguo wa Bahari Hindi)
Wimbo wa taifa: Taifa
Lokeshen ya Mauritius
Mji mkuu Port Louis
20°10′ S 57°31′ E
Mji mkubwa nchini Port Louis
Lugha rasmi Kiingereza na Kifaransa ingawa si rasmi kabisa
Serikali Jamhuri
Prithvirajsing Roopun
Pravind Jugnauth
Uhuru
kutoka Uingereza
12.03.1968
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
2,040 km² (ya 169)
0.05
Idadi ya watu
 - Julai 2019 kadirio
 - 2013 sensa
 - Msongamano wa watu
 
1,265,475 (ya 156)
1,259,838
618/km² (ya 19)
Fedha Mauritian Rupee (MUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+4)
(UTC)
Intaneti TLD .mu
Kodi ya simu +230

-


Ramani ya kisiwa cha Morisi

Morisi ni nchi inayoitwa rasmi Jamhuri ya Morisi (kwa Kiingereza: Republic of Mauritius, kwa Kifaransa: République de Maurice). Ni nchi ya visiwa katika Bahari Hindi karibu na Afrika, takriban Km 900 mashariki kwa Madagaska na km 4000 kusini-magharibi kwa Bara Hindi.

Nchi ilipata uhuru tarehe 12 Machi 1968, ikawa jamhuri tarehe hiyohiyo mwaka 1992.

Jina linatokana na kisiwa chake kikubwa, lakini eneo la jamhuri ni pamoja na kisiwa cha Rodrigues, visiwa vidogo vya Cargados Carajos na Agalega.

Hivyo vyote ni sehemu ya funguvisiwa la Maskarena pamoja na kisiwa cha Réunion ambacho ni mkoa wa Ufaransa.

Mji mkuu wa jamhuri ni Port Louis.


Morisi

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne