Mugumu

Mugumu
Mugumu is located in Tanzania
Mugumu
Mugumu

Mahali pa Mugumu katika Tanzania

Majiranukta: 1°50′21″S 34°40′28″E / 1.83917°S 34.67444°E / -1.83917; 34.67444
Nchi Tanzania
Mkoa Mara
Wilaya Serengeti
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 13,288

Mugumu ni mji mdogo na makao makuu ya Wilaya ya Serengeti katika Mkoa wa Mara, Tanzania, yenye postikodi namba 31601.

Ni nyumbani kwa hifadhi maarufu Duniani Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 13,288 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ya Mugumu ilikuwa na wakazi wapatao 10,226 waishio humo. [2]

Wakazi wengi wa Mugumu ni Wakurya; pia kuna makabila mengine kama vile Waikoma, Wanata, Waisenye, Wakisii na wengine wengi wanaofanya mji huo kuwa na mchanganyiko wa makabila.

Zaidi ya asilimia 50 ya wakazi wa hapo ni waumini wa dini ya Kikristo.

  1. https://www.nbs.go.tz, uk 192
  2. Sensa ya 2012, Mara - Serengeti-District-Council

Mugumu

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne